TMDA YATOA UFAFANUZI UVUMI WA DAWA YA PARACETAMOL INAYODAIWA KUBABUA NGOZI

2 months ago 159

MAMLAKA ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA)iliyo chini ya Wizara ya Afya, imetoa taarifa kwa Umma ufafanuzi kuhusu uvumi juu ya Dawa ya Paracetamol inayodaiwa kubabua ngozi.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo kwa Umma liyotolewa na Mkurugenzi Mkuu wa TMDA, Dkt. Adam Fimbo Imebainisha kuwa, imebaini uwepo wa taarifa inayosambazwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu uwepo wa dawa aina ya Paracetamol ambayo imeandikwa P 500 na 

kudaiwa kubabua ngozi kama inavyooneshwa (pichani).

Akinukuu taarifa hiyo inayosambazwa mitandaoni:

"Dawa hiyo inadaiwa kuwa ni ‘’paracetamol mpya nyeupe sana na inayong'aa, madaktari 

wanashauri kuwa ina virusi vya "Machupo", inayochukuliwa kuwa moja ya virusi 

hatari zaidi ulimwenguni, na kiwango cha juu cha vifo.

Aidha, Mtoa taarifa anaitaka jamii kuisambaza taarifa hii kwa kila mtu aliyeko katika orodha 

yake ya mawasiliano ili kuokoa maisha. Anamalizia kwa kusema ‘’Nimefanya 

sehemu yangu, sasa ni zamu yako. Kumbuka kwamba Mungu huwasaidia wale 

wanaosaidia wengine. ‘’Sambaza kama ilivyopokelewa’’.

Dkt.Fimbo ameeleza kuwa, Taarifa hiyo imekuwa ikijirudia mara kwa mara na TMDA imekuwa ikitolea ufafanuzi ikiwemo taarifa ya mnamo tarehe 10 Mei, 2023, juu ya dawa aina ya P-500® 

(PARACETAMOL) ya Apex Laboratories Private Limited, Tamil Nadu, India 

iliyodaiwa kuwa na virusi hivyo.

"TMDA inapenda kuufahamisha Umma kwa mara nyingine kwamba hakuna virusi 

vinavyojulikana kwa jina la Machupo. Aidha, virusi vya aina yoyote haviwezi kuishi kwenye kidonge. 

Dawa zenye kiambata hai cha paracetamol inayotumika kutibu homa na maumivu 

zilizopo katika soko nchini kwa majina mbalimbali ya kibiashara zimesajiliwa baada 

ya kuthibitishwa kuwa zinakidhi vigezo vya usalama, ubora na ufanisi unaotakiwa na 

hivyo, ni salama kwa matumizi yaliyoainishwa. 

Katika hatua hiyo, TMDA inapenda kuwahakishia wananchi kuwa inaendelea kutimiza wajibu wake wa 

kulinda afya ya Jamii kwa kuhakikisha kuwa bidhaa tiba zinazotumika nchini ni zile 

zenye kukidhi matakwa ya ubora, usalama na ufanisi.

Vilevile, Mamlaka inapenda kuwakumbusha wananchi umuhimu wa kupata ufafanuzi 

kutoka kwenye mamlaka husika kabla ya kusambaza taarifa zinazoweza kuleta 

taharuki kwenye Jamii.

TMDA yenye jukumu la kudhibiti ubora, usalama na ufanisi wa bidhaa tiba nchini ambapo Ili kuhakikisha kuwa bidhaa tiba (zikiwemo dawa) zilizoko katika soko nchini zinakidhi matakwa ya usalama, ubora na ufanisi, TMDA imeweka mifumo mbalimbali  ya udhibiti ikiwa ni pamoja na tathmini na usajili, ukaguzi, uchunguzi wa kimaabara  na ufuatiliaji wa ubora na usalama wa bidhaa katika soko. 

Aidha, Wananchi wanaweza kupiga simu ya bila malipo: 0800110084 endapo wapatapo taarifa za mashaka kama hizo.

Source : Michuzi Blog

SHARE THIS POST